MHESHIMIWA JENISTA MUHAGAMA AFUNGA SEMINA YA SIKU 5 KWA VIONGOZI WA CCM WILAYA YA LUDEWA


Mbunge wa Jimbo la Ludewa  Ndugu Deo Filikunjombe akizungumza na Viongozi wa CCM Wilaya ya Ludewa wakati wa kuhitimisha Semina ya Siku 5 ya Mafunzo kwa viongozi hao wa CCM iliyofanyika kwenye ukumbi wa Serengeti ,JB Belmont jijini Dar es Salaam.
Dk.Susan Kolimba akichangia mambo muhimu kwa viongozi wa CCM wilaya ya Ludewa wakati wa kuhitimisha mafunzo ya siku 5 kwa viongozi hao.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Muhagama akizungumza wakati wa kuhitimisha mafunzo ya siku 5 kwa viongozi wa CCM wilaya ya Ludewa yaliyoandaliwa na kuratibiwa na Mbunge wa Jimbo la Ludewa Ndugu Deo Filikunjombe.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Muhagama akisisitiza jambo wakati wa kufunga semina ya mafunzo kwa viongozi wa CCM wilaya ya Ludewa na kuwaambia Viongozi wa ngazi za chini wanaowajibu wa kusimamia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM.
Viongozi wa CCM Wilaya ya Ludewa wakimsikiliza Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Muhagama wakati wa kuhitimisha mafunzo ya siku 5 kwa viongozi hao ambao iliwajumuisha Wenyeviti, Makatibu na Makatibu Wenezi.
Washiriki wa Semina hiyo wakipiga makofi wakati wa kuhitimisha semina hiyo.
Mkufunzi wa Masomo kwa Viongozi wa CCM Wilaya ya Ludewa Ndugu Kilumbe Ng'enda akizungumza machache wakati wa kufunga semina hiyo kwenye ukumbi wa Serengeti uliopo kwenye Hotel ya JB Belmont jijini Dar-es-Salaam.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Muhagama akimkabidhi cheti cha kuhitimu mafunzo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ludewa Ndugu Stanley Kolimba (MB) Mstaafu.
Mbunge wa Jimbo la Ludewa Ndugu Deo Filikunjombe akimunyosha maneno yaliyoandikwa kwenye kofia Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Muhagama yanayosema Baki Njia Kuu wakati wa kuhitimisha mafunzo kwa viongozi wa CCM Ludewa.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Muhagama akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa CCM wilaya ya Ludewa baada ya kufunga mafunzo kwa viongozi hao kwenye hoteli ya JB Belmont jijini Dar Es Salaam.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Muhagama akiagana na Viongozi wa CCM Wilaya ya Ludewa baada ya kufunga rasmi semina ya siku 5 ambayo imewajenga viongozi wao kuwa na umoja na mshikamano na kuwapa uwezo wa kukiimarisha chama katika maeneo yao.
(Picha na Adam Mzee)

No comments:

Post a Comment