MO DEWJI ANYAKUA TUZO YA MWAKA YA MFANYABIASHARA ANAYESAIDIA ZAIDI JAMII

IMG_9463
Mkurugenzi Mtendaji wa CNBC Africa, Roberta Naicker akimkabidhi tuzo ya '2015 Philanthropist of the year-East Africa' Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji katika sherehe zilizofanyika hoteli ya DusitD2 jijini Nairobi.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).
IMG_9492
Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akizungumza kwenye hafla ya tuzo za All Africa Business Leaders Awards 2015 (AABLA). Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa CNBC Africa, Roberta Naicker.
IMG_9595
Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akipozi katika picha ya kumbukumbu na Mkurugenzi Mtendaji wa CNBC Africa, Roberta Naicker.
IMG_9627
Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akiwa ameshikilia tuzo yake.
IMG_9608
Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akibadilishana mawazo na baadhi ya wafanyabiashara wakubwa jijini Nairobi ambapo pia walimpongeza.
IMG_9587
Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji katika picha ya kumbukumbu na mmoja wa wageni waalikwa kwenye hafla ya tuzo za All Africa Business Leaders Awards 2015 zilizofanyika kwenye hoteli ya Dusit D2 jijini Nairobi.
IMG_9655
Mohammed Dewji, CEO of MeTL Group....2015 Philanthropist of the Year-East Africa.
Na Mwandishi Wetu
BILIONEA anayemiliki kampuni kubwa ya Mohammed Enterprises nchini (MeTL), Mohammed Dewji `Mo’ ameshinda Tuzo ya Mfanyabiashara wa Mwaka anayejitoa zaidi kuisaidia jamii kunufaika kutokana na biashara zake, akiwa mshindi wa Afrika, Kanda ya nchi za Afrika Mashariki katika tuzo zilizofanyika juzi jijini Nairobi, Kenya.
Katika tuzo hiyo ya heshima kwa wafanyabiashara Afrika inayoratibiwa na Kituo cha Biashara cha Televisheni ya CNBC Afrika, Dewji alishindanishwa na mabilionea raia wa Kenya, Ashok Shah wa kampuni ya Apollo Investment Limited na Damaris Too-Kimondo anayemilikia kampuni ya Shrand Promotions.
Katika sherehe hizo zilizofana, Dewji alikabidhiwa tuzo yake na Mkurugenzi Mtendaji wa CNBC Africa, Roberta Naicker.
Ushindi wake umechangiwa kwa kiasi kikubwa na kitendo cha Dewji ambaye pia ni mwanasiasa aliyekuwa mbunge wa Singida Mjini kwa miaka kumi, kujihusisha na misaada yenye lengo la kupambana na umasikini kupitia sekta mbalimbali kama elimu, maji, watu wenye ulemavu na pia uwezeshaji kiuchumi, matukio ambayo yamelenga na kubadili hali ya watu maskini zaidi katika jamii.
Washindi hao wa Kanda ya Afrika Mashariki watashindanishwa na washindi wengine kutoka Kanda ya Kusini mwa Afrika na Afrika Magharibi Novemba 13, mwaka huu huko Sandton, Johannesburg nchini Afrika Kusini ili kupata mshindi wa jumla wa bara la Afrika.
Akizungumza mara baada ya kutunukiwa tuzo yake hiyo yenye heshima kubwa, aliwashukuru waandaaji, jarida la Forbes na majaji kwa kumuona anastahili kwa tuzo hiyo ya kipekee.
Alisema, kwake ni faraja kubwa kupata heshima huyo na amekuwa na ndoto za kusaidia watu wa Tanzania kukabiliana na changamoto wa kasi ya maendeleo barani Afrika na kwamba ili kuendana na kasi hiyo, miongoni mwa juhudi zinazotakiwa ni kuwawezesha kupata elimu bora, hasa wa maeneo ya vijijini.
“Ninaamini tukiunganisha nguvu, nchi za Afrika zina nafasi kubwa ya kuwa na wataalamu wake watakaosaidia kusukuma gurudumu la kiuchumi Afrika na hivyo kuboresha hali za maisha za watu wa bara hili,” alisema bilionea huyo kijana aliyeanzishwa taasisi yake ya Mo Dewji Foundation kwa lengo la kuisaidia jamii.
Alisema kwamba hilo ni tukio kubwa sana kwake na kumnukuu Maya Angelou, akisema: “Ukisoma, fundisha. Ukipata, toa.” Aliongeza kuwa, kwa kuwa amebarikiwa na Mungu kupata vyote, anakusudia kuendelea kuuelimisha umma juu ya kufanya mapinduzi ya kielimu, afya, na maeneo mengine ya ustawi wa jamii, huku akiahidi kusaidia kwa kila atakachojaliwa.
Dewji mwenye umri wa 40 ambaye kwa sasa ndiye bilionea kijana zaidi Afrika kwa vijana wasiozidi umri huo, akiwa pia miongoni mwa mabilionea 55 wanaoongoza kwa utajiri Afrika, anaongoza kampuni yenye makampuni yaliyojikita katika sekta za kilimo, fedha, uzalishaji, usambazaji wa bidhaa na kadhalika, huku akitajwa kuajiri zaidi ya watu 20,000.

Katika "HUYU NA YULE" ya NJE-NDANI wiki hii......



Photo Credits: Bongo Celebrity 
Katika NJE NDANI wiki hii, mbali na habari kutoka Afrika, utasikia mahojiano yangu na NURU THE LIGHT.
Msanii, Mjasiriamali, Mtangazaji, Blogger na Mwanaharakati ambaye amekuwa mkarimu sana kujiunga nami kutoka Stockholm Sweden
Kazungumza mengi mema
Jiunge nami, MUBELWA BANDIO Jumamosi (June 28) katika NJE NDANI ya Kwanza Production na Border Radio kuanzia saa sita mpaka saa nane mchana kwa saa za Marekani ya mashariki kupitia www.kwanzaproduction.com ama www.bordermediagroup.com

FILAMU YA ESPINHO DA ROSA “THE THORN OF THE ROSE” YATWAA TUZO TATU TAMASHA LA 17 LA ZIFF 2014


DSC_0987
Malkia wa Filamu ya Espinho da Rosa (the Thorn of the rose) ya Filipe Henriques kutoka Guinea Bissau ADY de Batista akiwasili huku akiongozana na Meneja wake Sholey Maqueta kwenye usiku maalum wa tuzo wakati wa tamasha la 17 la ZIFF 2014 lililomalizika mwishoni mwa juma visiwani Zanzibar kwenye viunga vya Ngome Kongwe.(Picha zote na Zainul Mzige wa MOblog).
Na Mwandishi wetu, Zanzibar
FILAMU ya Espinho da Rosa (the Thorn of the rose) ya Filipe Henriques kutoka Guinea Bissau imeondoka na tuzo tatu katika tamasha la 17 la filamu la kimataifa la Zanzibar (ZIFF).
Tuzo hizo ni pamoja na ya Signis , tuzo ya majaji na tuzo ya fedha ya ZIFF.
Katika tamasha hilo filamu iliyotwaa tuzo ya dhahabu ni ile ambayo ilikataliwa kuoneshwa nchini Nigeria ilikotengenezwa ya Half of a Yellow Sun iliyoongozwa na Biyi Bandele.
Shughuli za utoaji tuzo ambazo zilitanguliwa na hotuba ya makamu mwenyekiti wa kampuni ya wananchi Group ambayo brand yake ya zuku ndio inafadhili ZIFF pamoja na tuzo zake za Swahili, zilinogezshwa na vikundi mbalimnbali kikiwemo cha kereografu cha B 6.
DSC_0995
Mkurugenzi Mtendaji wa Hoteli ya Doubletree by Hilton Zanzibar, Bw. Samuel(kulia) Bond na Mkewe Jenny Bond wakibadilishana mawazo na mmoja wa majaji wa tuzo za ZIFF 2014 Mykel Parish (aliyeipa mgongo kamera) kabla ya kuanza kwa tuzo za ZIFF 2014.
Aidha mwenyekiti huyo alisema kwamba Zuku itaendelea kuhakikisha inasaidia kuinua kiwango cha uigizaji na utengenezaji sinema za Kiswahili kwa kutambua kwamba filamu hizo ni sehemu ya uzalishaji wa fedha katika taifa kupitia utamaduni.
Aidha alisema pamoja na mamilioni ya shilingi walioyoahidi kutumbukiza katika miaka 10 ni vyema taasisi nyingine hasa za umma kutambua uwapo wa tamasha hilo ambalo likitumika vyema ni chanzo kikuu cha fedha kwa serikali na watu wake.
Katika utoaji wa tuzo ambao ulionekana nchi ya Afrika Kusini kufanya vyema, mtendaji wa ZIFF Professor Martin Mhando alizungumza maana ya nchi za majahazi na nini kinastahili kufanywa.
DSC_1071
Mkurugenzi Mkuu wa ZIFF, Profesa Martin Mhando akiwakaribisha wageni waalikwa waliohudhuria usiku maalum wa tuzo za tamasha la 17 la ZIFF 2014 zilizofanyika mwishoni mwa juma.
Alisema tamasha hilo halitabadili wajibu wake wa tangu awali wa,mkuchochea mabadiliko miongoni mwa jamii na serikali hali ambayo inajenga jamii yenye kuheshimu maendeleo na wajibu wa kila mmojawao.
Alisema pamoja na kuwa na safari ndefu bado ZIFF ndio jukwaa lenye uhakika kwa watengeneza sinemakatika bara la Afrika na kadhalika.
Katika utoaji tuzo,ZIFF ilialika zaidi ya watengeneza filamu 30 kutoka nchi mbalimbali.
ZIFF 2014 – AWARDS
SIGNIS AWARDS
SPECIAL MENTION
Shadow Tree
By BIja Viswa
(Tanzania)
EAST AFRICAN TALENT AWARD (1000 dollars)
Sticking Ribbons
by Bill Jones
(Kenya)
SIGNIS PRIZE
Espinho Da Rosa/ The Thorn Of The Rose
by Filipe Henriques
(Guine Bissao)
SEMBENE OUSMANE AWARDS
Umunthu,
by Mwizalero Nyirenda
(Malawi)
Body Games,
by Richard Pakleppa& Matthias Rohrig Assuncao
(Namibia / Brasil / South Africa)
SPECIAL MENTION
Welcome to Loliondo
by Morten West
(Denmark)
ZUKU BONGO MOVIES AWARDS
ZUKU PEOPLE CHOICE
Shikamoo Mzee
DSC_1085
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wananchi Group ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo, Bw. Richard Bell akizungumza na wageni waalikwa wakati utoaji tuzo za ZIFF 2014 lililomalizika mwishoni mwa juma visiwani Zanzibar. Aidha mwenyekiti huyo alisema kwamba Zuku itaendelea kuhakikisha inasaidia kuinua kiwango cha uigizaji na utengenezaji sinema za Kiswahili kwa kutambua kwamba filamu hizo ni sehemu ya uzalishaji wa fedha katika taifa kupitia utamaduni na kutoa wito kwa wasanii wa Bongo Movie kupeleka kazi zao kwa ajili ya kuonyeshwa kwenye chaneli za ving'amuzi vya ZUKU na kujitangaza kimataifa kupitia ving'amuzi hivyo.
BEST ACTOR
Jackson Kabirigi
for Kisate and Nguvu ya Imani
BEST ACTRESS
Esha Buheti
for Mimi na Mungu wangu
BEST DIRECTOR
Issa Musa Cloud
for Shahada
BEST FEATURE FILM
Shahada
Issa Musa
ZIFF AWARDS
LIFETIME ACHIEVEMENT AWARD
Emerson Skeens
Founder of ZIFF
Awarded Posthumously
BEST DOCUMENTARY
Sobukwe: A Great Soul
Mickey Madoda Dube
(South Africa)
BEST ANIMATION
Khumba
Anthony Silverston
(SouthAfrica)
BEST SHORT FILM
Shadowtree
Mti Wakivuli / Biju Viswanath
(India / Tanzania)
BEST EAST AFRICAN TALENT
The King’s Virgin
Daniel Moss
(Tanzania/UK)
DSC_1118
Mmoja wa majaji wa tuzo za Signs kwenye tamasha la ZIFF 2014, Adinda Pamela akitangaza washindi wa tuzo hizo. Katikati ni Mratibu wa Majaji wa tuzo za ZIFF 2014, Fabrizio Colombo na kulia ni mmoja wa "ushers" akiwa ameshikilia tuzo hiyo.
CHAIRMAN’s AWARD
Sodiq
Adeyemi Michael
(UK)
SPECIAL JURY AWARD
Julio Mesquith
Main Actor
The Thorn of the Rose
BEST FEATURE FILM (SILVER DHOW)
The Thorn of the Rose - Espinho da Rosa
by Filipe Henriques (Guinea Bissau)
BEST FEATURE FILM (GOLDEN DHOW)
Half of a Yellow Sun
Biyi Bandele (USA)
DSC_1159
Mmoja wa washindi wa tuzo za Signis alikuwa ni ADY de Batista malkia wa Filamu ya Espinho da Rosa (the Thorn of the rose). Pichani ni ADY de Batista akisindikizwa jukwaani kupokea tuzo na Meneja wake.
DSC_1160
Mmoja wa majaji wa tuzo za Signis Adinda Pamela akimpongeza ADY de Batista baada ya kunyakua tuzo hizo.
DSC_1171
ADY de Batista akiongea kwa furaha kwenye usiku maalum wa tuzo za Signis katika kusheherekea tamasha la 17 la ZIFF lililomalizika mwishoni mwa wiki visiwani Zanzibar.
DSC_1175
DSC_1202
ADY de Batista akishuka jukwaani baada ya kupokea tuzo na Meneja wake.
DSC_1221
Channel Coordinator wa ZUKU Swahili, Bilha Olimba akitangaza jina la mshindi wa tuzo za ZUKU PEOPLE's CHOICE. Katikati ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Wananchi Group ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo kupitia brand ya ZUKU, Bw. Richard Bell
DSC_1223
Msanii wa filamu nchini Shamsa Ford akielekea jukwaani kumchukulia msanii mwezake Jacob Steven almaarufu kama JB alitwaa tuzo ya ZUKU PEOPLE'S CHOICE kupitia filamu yake ya SHIKAMOO MZEE kwenye tamasha la 17 la ZIFF lililomalizika mwishoni mwa juma visiwani Zanzibar.
DSC_1231
Shamsa Ford akizungumza kwa niaba ya JB kabla ya kupokea tuzo hiyo.
DSC_1241
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wananchi Group ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo kupitia brand ya ZUKU, Bw. Richard Bell akikabidhi tuzo ya ZUKU PEOPLE's CHOICE kupitia filamu ya SHIKAMOO MZEE ya mwigizaji Jacob Steven almaarufu kama JB iliyopokelewa na msanii mwenzake Shamsa Ford.
DSC_1245
Shamsa Ford akishukaa jukwaa kwa furaha isiyona kifani.
DSC_1267
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wananchi Group ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo kupitia brand ya ZUKU, Bw. Richard Bell akimkabidhi tuzo mwigizaji bora Jackson Laurent Kabirigi kupitia filamu ya "Kisate na Nguvu ya Imani" (wa pili kushoto) aliyeambatana na ndugu yake Feysal Arikardy (kushoto).
DSC_1283
Mtayarishaji wa filamu Swahiliwood, William Mtitu akielekea jukwaani kumpokelea tuzo mwongozaji wa filamu Issa Mussa a.k.a Cloud 112 aliyetwaa tuzo ya uongozaji bora kupitia filamu yake ya SHAHADA ndani ya tamasha la 17 la ZIFF 2014.
DSC_1285
Kwa picha zaidi ingia hapa

RAIS KIKWETE KUHUDHURIA MKUTANO WA 23 WA UMOJA WA AFRIKA


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa katika uwanja wa ndege wa Malabo, Equatorial Guinea, leo Juni 24, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Waziri Mkuu wa Equatorial Guinea Mhe Vicente Ehate Tomi alipowasili  katika katika uwanja wa ndege wa Malabo, Equatorial Guinea, Juni 24, 2014

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewasili mji mkuu wa Equatorial Guinea wa Malabo  Juni 24, 2014 kuhudhuria Mkutano wa Umoja wa Africa – African Union (AU).
Akiwa Malabo, Mheshimiwa Rais Kikwete pia atakuwa Mwenyekiti wa kikao cha wakuu wa nchi wanachama wa AU kitakachojadili mazingira. Rais Kikwete na ujumbe wake anatarajiwa kurejea nchini mwishoni mwa wiki.


DAR ES SALAAM KUWA KIVUTIO KIKUBWA CHA WAWEKEZAJI NA UTALII MIAKA MICHACHE IJAYO


 Pichani ni Jengo litakalojengwa jijini Dar es salaam na litagharimu Dola za kimarekani milioni 77,kutakuwa na hoteli ya hadhi ya Nyota Tano, Ofisi za Biashara, kutakuwa na Sehemu ya kuegesha magari, jengo hili litatakuwa kivutio kwa Wawekezaji na Utalii.
(23 Juni 2014)
 Baadhi Malori na Vifaa vingine vya kutendea kazi vikiwa tayari kuahiria ujenzi huu unaanza mara moja baada ya zoezi la uwekaji wa jiwe la msingi kukamilika.

 Mama Maria Nyerere akiwasili kwenye sherehe ya uwekaji jiwe la msingi wa ujenzi wa jengo la Malimu Nyerere Foundation Square
 Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mheshimiwa Benjamini Mkapa akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu Ndugu Cleopa Msuya wakati wa shughuli za uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi wa jengo refu la ghorofa la Mwalimu Nyerere Foundation.
 Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao (kushoto) na Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda (kulia) kwa pamoja wakifunua kitambaa kuashiria kuwekwa jiwe la msingi katika eneo litakapojengwa jengo la Taasisi ya  Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
  Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao (kushoto) na Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda (kulia) wakijippongeza baada ya kuweka jiwe la msingi katika eneo litakapojengwa jengo la Taasisi ya  Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao (katikati) na Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda (wa pili kulia) kwa pamoja  wakimwaga mchanga kuashiria kuanza kwa ujenzi jengo la Taasisi ya  Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam,Kulia ni Balozi wa China nchini Tanzania Lu Youqing na Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akibadilishana mawazo na Profesa Shivji pamoja na Wazee wengine wakati wa shughuli za uwekaji wa jiwe la msingi wa Ujenzi wa jengo la Mwalimu Nyerere Foundation Square.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku akihutubia wakati wa Uwekaji wa jiwe la msingi wa jengo la Mwalimu Nyerere Foundation Square.


Picha ya Pamoja baada ya zoezi la uwekaji wa jiwe la Msingi kukamilika.
(Picha na Adam Mzee)

MANISPAA YA ILALA YASAINI MKATABA WA BILIONI 2.1 KWA AJILI YA UJENZI WA MRADI WA MAJI KATA ZA KIVULE NA KIPUNGUNI


 Meya Wa Ilala Mh Jery Silaa Akiwasili kata ya Kipunguni na kupokelewa na Diwani wa kata Hiyo Na Viongozi wengine .
 Mkandarasi wa kampuni Kika Construction Mbaraka Kihawe akimkaribisha Meya Wa Ilala Mh Jery Silaa kwenye meza kuu.
 Mwanainchi Huyu alipatwa na Furaha sana Kumuona Mh Jery Silaa akashindwa kujizuia na kwenda Kumsalia.
 Wageni waliokuja kuhudhuria utiaji sahihi wa mikataba baina ya manispaa ya Ilala na Wakandarasi wakiwa meza kuu

Kaimu Mkuu wa Idara ya Maji Bi Selestina John akiongelea jinsi mradi huo wa maji kwa kata mbili za Kivule na Kipunguni ni namna gani zitanufaika na mradi huo mara tu baaada ya kukamilika mwezi wa kumi na mbili.Ambapo kwa kata ya Kivule wataweza kupata maji lita laki nne na themanini(480000) kwa siku,wakati kata ya Kipunguni B wataweza kupata maji lita  laki mbili na themanini na tano elfu(285,000) kwa siku.



 Diwani wa Kata ya Kivule Mh Nyasika Getama Akishukuru manispaaa kwa kuweza kuikumbuka kata yake katika mradi huo mkubwa wa maji kwa kata Hizo mbili
Mwakilishi wa Diwani wa kata ya KipunguniB akishukuru pia kwa kuweza kupewa mradi wa maji kwenye kata yao ya kipunguni B


 Meya wa Manispaa ya Ilala Mh Jerry Silaa akielezea ni kwani wameamua kuja kutiliana sahihi mbele ya wananchi ili kuweka uwazi na uwajibikaji wa kila mmoja,kuanzia Manispaaa mpaka kwa Wakandarasi.Hivyo amewataka  Wakandarasi hao kuwa makini na kufanya kazi kwa viwango ili kuweza kutatu Tatizo la Maji katika kata Hizo mbili.
Zoezi la utiaji Saini likiendelea
 Mkandarasi kutoka Kika Construction Mbaraka Kihawe wa pili kutoka kushoto akitia sahihi mkataba wa ujenzi wa mradi wa Maji kata za Kipunguni B na Kivule na Manispaa ya Ilala,Meya Wa Manispaa ya Ilala(mwenye miwani)akishuhudia Mwanasheria wa Manispaa Kulia akitia sahihi Mikataba Hiyo.
Mwanasheria wa Manispaa Mashauri Musini Kulia akitia sahihi Mikataba Hiyo Huku akishuhudiwa na Viongozi wa kata za Kipunguni B na Kivule.
 Mkandarasi wa Kampuni ya JP Traders  wa Pili kutoka Kushoto akitia sahihi mkataba wa ujenzi wa mradi wa maji baina yake na Manispaa Ya Ilala,Kulia ni mwanasheria wa Manispaa ya Ilala Mashauri akihakiki na kutia sahihi mikataba hiyo.
 Meya Wa manispaa ya Ilala Mh Jery Silaa akikabidhiana Mikataba na Mkandarasi kwa Ajili ya mradi wa maji kwa kata za Kipunguni B na Kivule
Wanainchi wa kata Za Kivule na Kipunguni B wakifuatilia utiaji sahihi wa mikataba hiyo kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa Maji.PICHA ZOTE NA DJ SEK BLOG