MATUKIO MBALIMBALI YA ZIARA YA KATIBU MKUU RORYA

 Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Shiratu Obwere wilaya ya Rorya mkoa wa Mara.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Shiratu Obwere katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na maelfu ya watu.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akipiga gitaa wakati wa uzinduzi wa mradi wa bwawa la maji ya safi ya matumizi ya binadamu na kunyweshea mifugo kata ya Rocha.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda nyasi katika (lambo) bwawa la maji linalojengwa katika kata ya Rocha,wilaya ya Rorya.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye  akiwa ameketi pamoja na wajumbe wa shina namba 12 kata ya Utegi tayari kwa kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kubeba matofali kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya Tawi la Nyanduga.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo ya Daraja la Asili la Lorbimbe kutoka kwa mbunge wa Rorya Ndugu Lameck Airo.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wakazi wa kijiji cha Bukura baada ya kukagua ujenzi wa Maabara,Madarasa na Nyumba za walimu katika shule ya Sekondari Bukura.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kata ya Tai kijiji cha Masonga baada ya kuzindua mradi wa ujenzi wa nyumba ya Kikundi cha akina Mama  cha Upendo Women Group Masonga.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimbeba mmoja ya watoto yatima wanaolelewa na kituo cha  akina mama cha Upendo Women Group.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka jiwe la msingi wa ujenzi wa Hostel ya chuo cha waganga wasaidizi cha RAO HEALTH TRAINING CENTER.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa chuo cha RAO HEALTH TRAINING CENTER
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa RAO HEALTH TRAINING CENTER ,mwenye kofia ni Mkuu wa chuo hicho Dk. Ziki Makoyo.

No comments:

Post a Comment