KINANA AKOMAA MAWAZIRI

  • Sasa kuongozana na Mawaziri mguu kwa mguu
  • Asema kazi yake ya kuijenga chama inahitaji watu makini kama mtu hawezi kasi yake awapishe.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikaribishwa kwa kahawa katika kijiji cha  Budalabujiga wilaya ya Itilima mkoani Simiyu ambapo Katibu Mkuu alifanya ziara ya siku moja wilayani hapo.
  Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akikaribishwa kwa kahawa katika kijiji cha  Budalabujiga wilaya ya Itilima mkoani Simiyu, Katibu wa Itikadi na Uenezi ameongozana na Katibu Mkuu wa CCM katika ziara ya mkoa wa Simiyu.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akipata maelezo wakati akikagua Bwalo la chakula la shule ya sekondari ya kata ya Kanadi, wilayani Itilima mkoa wa Simiyu.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya kata ya Kanadi baada ya kutembelea bwalo na bweni la shule hiyo ambapo aliwasihi wanafunzi kusoma kwa bidii na kuahidi kuwapatia sola.
 Katibu Mkuu wa CCM akiwa amembeba mtoto Dhahabu katika kituo cha afya cha Nangale wilaya ya Itimila mkoani Simiyu.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye mavazi yake ya uchifu baada ya kusimikwa Uchifu na kutambulika kama Chifu Machibola katika kijiji cha Migato wilaya ya Itilima mkoa wa Simiyu, Katibu Mkuu yupo kwenye ziara ya mkoa wa Simiyu ambapo moja ya lengo la ziara yake ni kukagua na kuimarisha uhai wa chama na kusimamia ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2010.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akinywa maji kwa kutumia kipeyu katika kijiji cha Migato wilaya ya Itilima mkoa wa Simiyu.
 Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo ya ujenzi wa ofisi za halmashauri ya wilaya mpya ya Itilima kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri Dk. Leornard Masale
 Katibu Mkuu ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupiga lipu kwenye ujenzi wa ofisi za Halmashauri za wilaya ya Itilima mkoani Simiyu.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda mti kwenye uwanja wa ofisi za halmashauri ya wilaya ya Itilima mkoani Simiyu.
 'SIASA CHINI YA MTI' Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wajumbe wa halmashauri ya CCM wilaya ya Itilima kama sehemu ya kujenga na kukiimarisha chama.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Itilima katika viwanja vya Gangabilili na kuwaeleza wananchi wa eneo hilo kuwa mipango ya kuijenga wilaya hiyo inaendelea na CCM itasaidia sana katika kuleta mabadiliko ya kiuchumi hasa kwa wakulima wa zao la pamba na wafugaji.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa wilaya ya Itilima katika viwanja vya Gangabilili na kuwaambia wananchi hao muda wa viongozi kukwepa kutatua kero umekwisha na kuwataka viongozi kuwajibika moja kwa moja na kuahidi kuwa atakuja mkono kwa mkono na Waziri wa Nishati na Madini pamoja na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya makazi kutatua mgogoro mkubwa wa wafugaji na hifadhi pamoja na wakulima.
Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahma Kinana akipokea kadi kutoka vyama mbali mbali ambao wemerudi CCM zaidi ya watu 120 wamerudisha kadai katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Gangabilili willaya ya Itilima mkoani Simiyu.

No comments:

Post a Comment