KATIBU MKUU MSTAAFU WA UVCCM TAIFA LEO ALIPOKABIDHI OFISI HIYO RASMI KWA KATIBU MKUU MPYA!!


Thursday, September 5, 2013
 KATIBU Mkuu mstaafu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Martine Shigela (kushoto) akimkabidhi Katibu Mkuu mpya wa UVCCM, Sixtus Mapunda, faili wakati wa makabidhiano ya Ofisi, waliyofanya leo, Makao Makuu ya UVCCM, mjini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia ni, Naibu Katibu Mkuu UVCCM (Bara), Mfaume Ally Kizigo na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Utekelezaji UVCCM Taifa, Seki Kasuga..
 Sixtus Mapunda akipitia nyaraka kwenye faili alilokabidhiwa na Shigela wakati wa makabidhiano ya ofisi leo. Kushoto ni Kizigo
 Makamu Mwenyekiti UVCCM, Taifa, Mboni Mhita (kushoto) akisalimiana na Shigela baada ya kuwasili kwenye mapokezi hayo.
Mboni Mhita akimsalimia pia, Mkumbe wa Kamati Kuu ya Utekelezaji UVCCM Taufa,Seki Kasuga wakati wa makabidhiano hayo. Imetayarishwa na BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment